Project Hope     home >> stonecroft>>roho mtakatifu yuko wapi?>>somo la kwanza 1
Stonecroft - Roho Mtakatifu yuko wapi? - Somo la kwanza (#1)
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

ROHO MTAKATIFU YUKO WAPI?

SOMO LA KWANZA (1)

KUTAMBUA UWEPO WA ROHO MTAKATIFU

Lucille Sollenberger. B.S., M. A.

Stonecroft Ministries
www.stonecroft.org
P.O.Box 9609, Kancas City, MO 64134-0609

Download Full Swahili Guidebook

Download Swahili Guidebook Introduction

Download Swahili Lesson #1 Guidebook

Download Swahili Guidebook Front and Back page of folder

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #1

Mistari ya Biblia

LENGO LA SOMO
• Jifunze Roho Mtakatifu ni nani hasa.
• Kubali kazi za Roho Mtakatifu katika kufanya mahitaji yetu na wokovu wetu uweze kufanikiwa.
• Kujifunza kuwa Roho Mtakatifu anakuja ndani yetu pale ambapo tunampokea Roho Mtakatifu.
• Kujua kuwa waamini wote wana Roho Mtakatifu iwe wanajitambua au hawajitambui kuwa wana Roho Mtakatifu.

Somo hili ,linaelezea vizuri sana kuhusu wokovvu na jinsi ya kuwa mkristo. Itakuwa vizuri zaidi endapo tutakuwa na swali la kusema kuwa je unaamini?

Katika kuanza somo anza kwa kuwakaribisha watu kwa muda muafaka na waruhusu wao wenyewe katika kujitambulisha wao wenyewe.

MAOMBI
Baba uliyejuu mbinguni, tumekuja kujifunza neon lako.Tusaidie kuelewa tunapoendelea kujifunza. Ongeza upeo wetu ili tuweze kuona uwepo wako katika ukuu wako mwenyewe, na kuona upendo wako kwetu na huruma zako, tu naomba katika jina la Yesu Kristo….. AMEN

“Hakuna sehemu ya maisha ya mkristo ambayo hayajatawaliwa na kuwezeshwa na Roho Mtakatifu”
—John MacArthur.

Mwalimu wa Biblia John MacArthur ansema kuwa kila sehemu ya maisha ya mkristo inawezeshwa na ROHO MTAKATIFU.

Kwa kuwa huu ni ukweli, ni vizuri kusoma sana kuhusu Roho Mtakatifu, ambaye anafanya kazi kama vile anavyo fanya Mungu baba, na Yesu Kristo ambaye ni mwana. Pia tunatakiwa kutambua kuhusu ushiriki war oho Mtakatifu katika maisha ya mtu binafsi.

ROHO MTAKATIFU NI NANI?

Unaweza ukawa unajiuliza sana, Roho Mtakatifu ni nani?

Roho Mtakatifu yeye ni anaishi, na ni sawa na Mungu baba na Yesu mwana.

Yeye ni Mungu na ana kila sifa ya uungu.

Angalia katika swa;li la kwanza, na tutaangali Biblia inasema nini kuhusu Roho Mtakatifu.

Waweke washiriki pamoja na waweze kusoma na kujibu swali la kwanza. Wape muda ili waweze kuandika majibu yao katika vitabu vyao vya kujifunzia.

1. Kabla Yesu hajasurubiwa, aliwaambia wanafunzi wake kwamba kabla hajaondoka, mtu mwingine atatumwa kwa jina lake, soma katika Yohana 14:26……..

(Use your Bible or Africa Bible Verse Handbook)

a) Ni majina yapi mawili ambayo Yesu alimpa mtu huyo aliyekuwa anamsema……..
(Msaidizi na Roho Mtakatifu)
b) Nani alimtuma Roho Mtakatifu?........(Mungu Baba)
c) Mstari huu u nasema nini, kuwa atafanya nini?.........(Atafundisha wanafunzi na kuwakumbusha kile ambacho Yesu alisema).

Roho Mtakatifu ni mtu. Tunapofikiri kuhusu mtu, tunaangalia taswira yake ilivyo. Lakini kuna ugumu sana katika kujua taswira ya Roho Mtakatifu kwa sababu Roho Mtakatifu yeye hana mwili.

Wengi wetu hatuna tatiizo la kufikiria kuwa kuwa Yesu kama mtu. Tunajua kuwa Yesu alikuwa na mwili alipokuwa hapa duniani, hata hivyo hatuna ,maelezo ya kina kuhusu mw onekano wake. Pia vilevile ni vigumu kuiona taswira ya Mungu na Roho Mtakatifu kama wattu kwa sababu hawana miili kama ya wanadamu wengine.
Angali katika Yohana 4:24…….

Tuna weza kujifunza vitu viwili kutoka katika mstari huu:
• Mungu na Roho Mtakatifu wote ni Roho.
• Hatuwezi kumwabudu Mungu bila msaada wa Roho Mtakatifu.

Munu na Roho Mtakatifu wana haiba binafsi, lakini hawana sura au mwili ambayo unaweza kuiweka katika akili zetu.

Watu wengi wanafanya makosa kwa kumpa kikomo Roho Mtakatifu kwa kulazimisha, kwa nguvu N.K. kusema kuwa na nguvu, ushawishi N.K ni kuchukuahaiba yake na uwezo wake kufanya kazi ambazo mwanadamu anaweza kufanya. Roho Mtakatifu ni mtu roho.

Angalia katika swali la pili (2) na uone nini kitu kingine ambacho Biblia inasema kuhusu Roho Mtakatifu kama mwanadamu.

2. Roho Mtakatifu ni mtu. Mistari ya Biblia ifuatayo inathibitisha hilo.
Andika mstari sahihi baada ya kila sentensi.

Yohana 15:26………
Matendo ya mitume 13:2…….
Warumi 8:14……..
Warumi 8:26……..

a. Roho Mtakatifu huwa anaongea. (Matendo 13:2)
b. Anatuombea sisi. (Warumi 8:26)
c. Anafunua ukweli kuhusu Yesu Kristo. (Yohana 15:26)
d. Anawaongoza wana wa Mungu. (Warumi 8:14)



3.Yesu aliwaambi awanafunzi wake kwamba atawatumia msaidizi ambaye ni Roho Mtakatifu baada ya yeye kuondoka. Roho Mtakatifu alipokuja je alikuwa na dhumuni gani?

2 Wakorinthians 1:21-22………( Roho Mtakatifu anaingia ndani ya maisha ya kila muamini, kama garantii ya kwamba Mungu a nawamiliki, na ana Baraka nyingi juu yao amabzo amezihifadhi kwa wale wote wanaompokea yeye.)

Swali linalofuata linahusu nini ambacho Roho Mtakatifu anafanya kwa kila mtu.

4. Yesu alisema nini kuhusu Roho Mtakatifu (msaidizi) anachokifanya kwaq watu wa ulimwengu huu?.

Yohana 16:7-11…….( Roho Mtakatifu anaonesha na kufunua ukweli wa Mungu na kuwajulisha watu kuwa wanakosea wasipo muamini Mungu.)

Roho Mtakatifu anauhakikishia ulimwengu kuwa unakosea kuhusu wanaoamini kuhusu dhambi na hukumu. Isaya 5:20 inasema kuwa “ole wao wasemao uovu ni wema,na kwamba wema ni uovu,watiao giza badala ya nuru,na nuru badala ya giza,watiao uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu”

Roho Mtakatifu haendani kabisa na dhambi ambazo zinakuwepo nadani ya maisha yetu. Anatuambia kuwa sisi tumekosea, pale tunaposema kuwa Mungu ataziachilia mbali dhambi zetu. Inatakiwa tufikilie kuwa a namaanisha wale watu waovu ndio watakao hukumiwa, na sio sisi na anatuambia kuwa hukumu ipo inakuja.

Angalia ini Biblia inasema kuhusu hukumu katika ukurasa wa Waaamuzi 1:14-16……. Mungu ataleta hukumu kwa wote walio kinyume na yeye, na wale wote wanao wanaotenda maovu. Kwa maneno me ngine Mungu atawaadhibu wote wale ambao hawamuheshimu yeye.

Soma Warumi 6:23……..Mungu anasema kama tukitenda dhambi, tunatakiwa kufa kwa ajili ya kulipa juu ya dhambi hiyo. Bilia inatuambia kuwa hatuwezi kuingia mbinguni kama sisi hatupo katika familia ya Mungu. Kazi muhimu ya Roho Mtakatifu kwetu nikuwa sehemu yake ni kuzliwa kwetu upya. Anatukumbusha kuwa sisi ni watenda dhambi na ambao tulitakiwa kufa. Kwa hiyo tunataka mkombozi atakaye tuokoa katika dhambi ili tusifie katika dhambi hiyo.

KUPOKEA ROHO YA MUNGU

Tunapoamini ukweli kwamba kifo cha kristo pale msalabani kilikuwa ni kulipa deni ya dhambi zetu, tunamuomba Mungu msamaha ili atusamehe dhambi zetu na aweze kulinda maisha yetu. Katika wakati huo tunakuwa tumezaliwa katika familia ya Mungu na kupokea Roho Mtakatifu katika maisha yetu. Anachuklua nafasi ya kukaa katika maisha yetu kwa ajili yeye kutulinda kila siku.

5. a. Jinsi gani ambavyo tunazaliwa katika familia ya Mungu?
Yohana 3:5-7………….. (Kwa Roho ya Mungu, pia anaitwa Roho Mtakatifu.)

b. Tito 3:4-7……….(Roho Mtakatifu anatupa kuzaliwa upya na maisha kuyafanya kuwa mapya.)

Kuzaliwa upya ni kazi ya Roho wa Mungu. Inatokea mara kwa mara, na sio katika hatua hatua. Pale tunapogundua kuwa na mazingira magumu ya kuachwa na Mungu au kutengana na Mungu na kumuomba yeye ili atuokoe sisi Roho Mtakatifu wa munu anaingia nani yetu ammbapo anatupa maisha marefu na ambayo hayataisha leo wala kesho yaani ni ya milele.

Unapomwamini Yesu kama mwokozi wako, unapokea nini au unapata nini? Soma Yohana 3:16….. (Uzima wa milele na Mungu.)

6. Na ni aliyealikwa kuja kupokea zawadi ya ya maisha ya milele? Ufunuo 22:17…….. (Roho Mtakatifu anamkaribisha kila mtu kuja.)

Ingawa Roho Mtakatifu anawalika kila mtu, sio wote wanaobadilika na kuwa Wakristo. Kupokea wokovu ambao Yesu Kristo alitupa kupitia kifo chake, mapenzi ya mtu muhusika mwenyewe yanahusika. Hakuna mtu mwingine yeyote atakaye fanya uchaguzi huu, hapa kinachoangaliwa sana ni matakwa ya mtu binafsi.

Tunapojishusha kwa Mungu, anachukua maisha yetu ya dhambi na anatupa maisha ya utakaso yaaani ya utakatifu wa kristo. Kwa hili ili litokee, ni vizuri matakwa haya yaweze kuhusishwa.

Sisi tumeokoka au tunaokolewa pale tunapompokea Yesu Kristo. Hata kama sisi ni Wakristo, hatuoni vizuri Mwanzoni mwa maisha ya Ukristo. Maono yetu yamegubikwa na tabia ya dhambi, na kufikiria dhambi kila muda.

Maono hayo mabaya yanaondoka pale tunapoendelea kujifunza kuwa Biblia inatuambia nini. Tunatakiwa kuchagua kile tunachokisoma na kuweza kuhusisha kujitambua kwetu sisi kama sisi. Baada ya hapo tutajifunza jinsi ya kuishi maisha ya Kikristo ni hatua inayochukua muda mrefu sana.

Faida mojawapo ya kujifunza Biblia, ni jinsi ya kujifunza kutumia neno la Mungu katika maisha yetu ya kila siku. Katika kutumia masomo haya ya Roho Mtakatifu mtazamo wetu ndio unatakiwa kuwa yakinifu na sio tabia yetu. Kubadilisha mawazo ni vigumu sana kuliko kubadilisha tabia ya mtu.

MUNGU NI MMOJA

Majina na maandiko ya Roho Mtakatifu yanafunua uhusiano uliopo kati ya Mungu na Yesu Kristo. Soma Warumi 8:9 ,uoneshe majina mawili ambayo Roho Mtakatifu aliitwa…… (Roho ya Mungu na Roho ya kristo) kwa hiyo Roho Mtakatifu ana majina mengi sana ambayo ni tofauti tofauti.

Tunapo jifunza kuhusu Yesu Kristo, tunajifunza kuwa moja kati ya majina yake ni NIKO, ambapo Biblia ndiyo inayosema kuwa ni jina la MUNGU. Soma Yohana 10:30……. Hii itakuwa ngumu sana kwa fahamu zetu kuelewa .pia tunaposoma mistari inayozungumzia kuhusu Roho Mtakatifu na Mungu ni kitu kimoja, ni rahisi kuelewa kwa sababu wote hawa ni Roho.


Biblia inatufundisha tangu Mwanzo mpaka mwisho kuwa Mungu, Yesu na Roho Mtakatifu wana tabia moja. Ni kitu kimoja na kufanya kazi pamoja tena kwa umoja.

Tuna Mungu mmoja aambaye ana kazi tatu tofauTito fauti na katika yeye tuna uhusiana katika utatu.

Kwa yote kuelewa hili ni vigumu sana .Yesu yeye hana mwisho, laini mawazo yestu yana ukomo. Haiwezekani kumwelewa Mungu kuwa yukoje. Nahiyo ilikuwa nisababu mojawapo ya Mungu kumtuma Yesu ulimwenguni ili kuweza kutoa na kutujulisha asili ya Mungu na ukuu wake katika njia ambayo tunaweza kumuelewa.

Tunapomwamini Yesu kama mwokozi wetu, Mungu anatupa Roho wake ili kutufundisha na kutuongoza sisi. Tunapozidi kusoma na kujifunza neno la Mungu, ndivyo tutakavyoelewa umoja uliopo kati ya Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.

Roho Mtakatifu ana kila kitu cha uuungu ambacho Mungu anacho. Swali linalofuata linathibiftisha sifa zote hizo jinsi zilivyo.

7. Roho Mtakatifu anazo sifa zote ambazo Mungu na Yesu Kristo wanazo.
Sifa hizo tatu zipo zimeorodheshwa hapa chini katika mistari ifuatayo.

Sifa zifuatazo je zinadhihilrisha kuhusu rioho Mtakatifu?

Mpaji wa maisha
Anaishi milele
Maarifa yote, amniscience.

1 Korontho 2:11…….
(Maarifa yote - omniscience)

Waebrania 9:14…….
(Uzima wa milele)

Warumi 8:2,10……..
(Mpaji wa maisha)

Mungu alituokoa sisi kupitia Roho Mtakatifu, anyetupa kuzaliwa upya na kuwa na maisha mapya. Roho Mtakatifu anatuwezesha sisi kukamilisha mipango ya Mungu katika maisha yetu. Hatujui mipango ya Mungu kwamba ikoje, lakini tunapomkaribisha yeye ili awe ndani ya maisha yetu na kumruhusu kudhibiti maisha yetu, atatimiza mipango yake aliyoiweka juu yetu sisi.

Pale tunapokuwa Wakristo, tunashangazwa tunapoona kwa kujua, kuwa na Yesu katika maisha yetu kunabadilisha tabia zetu na pia inasababisha kufikiri kitofauti, tuna hamu ya kusikia kuwa Mungu anasema nini na kitu gani anakitarajia kutoka kwetu.

Mara nyingi tunafanya makosa katika kuangalia Wakristo wengine, na kuanza kushawishi maisha yetu badala ya yale ya kwao. Au tunaweza kusukumwa na kile watu ambao ni Wakristo wanachohitaji kutoka kwetu.

Inatakiwa twende ndani ya neno la Mungu na kusoma na kujua neno linasema nini kuhusu tunachotakiwa kukifanya na tunafanyaje. Tunatakiwa kuwa na hamu binafsi ya kukua kiimani na katika utii katika mwongozo wa Mungu Roho Mtakatifu. Atatusaidia katika kuelewa neno lake. Hii itatusaidia sisi katika kujizuia na watu kutaka kujua kile ambacho kipo ndani yetu, na sio vile Mungu anatarajia kutoka kwetu.

Wakati Yesu Kristo ni muhimiri wa maisha yetu na tunampenda sana kwa moyo wote. Na tunapotaka kufanya jambo Fulani ambacho hakihitaji uangalifu sana, mara zote akili zetu na mafikilio yetu yanaelekeza moja kwa moja kwenye maombi, au katika kuimba au kwenye nyimbo za kuabudu. Tunafikilia kkuhusu uhusiano wetu na Mungu au nini ambacho unaweza kumfanyia mtu ambaye tunatakia kumtumikia na tunataka kufikia pendo lake.

Majibu ya maswari 8 yatatofautiana,mpe kila mmoja nafasi ya kujieleza.

8. a. Je unatambuaje uwepo war oho Mtakatifu ndani yako na analeta madhara gani pale unaposema na unapofanya kitu Fulani?.....

b. Kuwa na utambuzi juu ya Roho Mtakatifu kuna athiri vipi muunganiko wako wewe na Yesu Kristo?.....

Tumia ukweli huu ndani ya aisha yako katika wiki hii, kuwa na ufahamu au fahamu kuwa Mungu yuko pamoja na wewe. Kuna kuwa na furaha isiyoelezeka pale unapoishi ndani ya ushirika wa Mungu.

Kwa kiurudia. Fikiria kuhusu tulichokisoma kuhusu Roho Mtakatifu:

Kutoka katika swali la 1:

Majina gani mengine ambayo Yesu aliweza alimpa Roho Mtakatifu?.....................(Msaidizi)

Nani alimtuma ………….(Mungu baba).

Alitakiwa kuja kufanya nini………(Kuwafundisha wanafunzi na kuwakumbusha kwa kile alichokisema Yesu)

Kutoka katika swali la 4 na la 5:

Je Roho Mtakatifu alihusika vipi kabla ya kuwa Wakristo?......(Sisi tulikuwa hatiana na alituonyesha kuwa sisi tunahitaji ukombozi ili tutoke katika dimbwi la dhambi tuliyonayo)

Kutoka katika majadiliano:

Ni wakati gani ambapo Roho Mtakatifu anaingia ndani ya maisha ya mtu?.......(Pale mtu anapokubali kumpokea Yesu Kristo kuwa bwana na mwaozi katika maisha yake)

Kuutoka katika swali la 7:

Tumejifunza kuwa Roho Mtakatifu ni mtu ambaye ana sifa kama zile alizonazo Mungu na Yesu Kristo. Hebu taja zile sifa tatu tulizozitaja walati tunajadili katika somo hili…..(Maarifa yote, uzima wa milele, na mpaji wa uzima)

Mmoja na anayeishi Mungu wetu wa mbinguni, muumbaji wa mbingu na dunia, alimtuma Roho wake Mtakatifu ili aweze kuingia ndani yetupale tunapompokea, anaigia kama zawadi ambayo Mungu anatupatia kwa ajili ya wokovu. Tunapomalizia tunaweza kumshuru Mungu kwa kutupa Roho Mtakatifu ambaye anatulinda.

Juma lijalo,somo 2 inatutamburisha katika juma la kujisomea biblia,kila siku,soma mstari wa biblia katika biblia yako au kitabu cha biblia ambacho kinakuja na masomo haya.biblia inaeleza sana kuhusu Roho mtakatifu na inajibu maswari mawili,tambua mambo mapya uliyojifunza kuhusu Mungu,katika kulasa ya mwisho.

MAOMBI

Baba yetu uliye mbinguni, asante kwa Roho wako Mtakatifu. Tusaidie sisi kumsikia rohoo Mtakatifu anapoongea nasi. Hatuwezi kusikia kila kitu tuliyoyaongea leo, lakini tunajua ya kuwa kitu ambacho tunatakiwa kujua sisi sota ni kuamini. Tusaidie sisi kujifunza nini kile tunachotakiwa kujua tutakapoendelea kujifunza na kusoma somo linalofuata wiki hii. Tunaomba katika jina la Yesu …….

AMEN

 

 
 

This is a translation of 'Who is the Holy Spirit?' Stonecroft's Guide Book Lesson #1 in Swahili, the English version of Who is the Holy Spirit? is available online from Stonecroft's website.

This transforming study will reveal who Jesus is, what He does, and what life is like when He lives within you. Learn what the Holy Spirit does in the life of a Christian and how He can help you grow to be more like Christ. (6 lessons)

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Full Swahili Guidebook

Download Swahili Guidebook Introduction

Download Lesson #1 Swahili Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #1

Download Swahili Lesson #1 Student Study Book

 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us