Project Hope     home >> stonecroft>>roho mtakatifut
Stonecroft - Roho Mtakatifut
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

MWONGOZO UTAKAOTUONGOZA KATIKA KUJIFUNZA MASOMO YA BIBLIA YA STONECROFT.

LENGO:

Kuwafikia: Masomo haya yanatuwezesha kupata njia ya kushirikiana kujua wokovu wa Yesu Kristo na watu wengine.kwa wale ambao wana makundi wanaombwa kualika marafiki zao, famila, wafanya kazi wenzao na pia majirani zao.

Uanafunzi: Wakristo wapya na wale waliokomaa wanaweza kusoma saaana kuhusu MUNGU na kuweza kukua naye katika uhusiano uliomzuri. Msomo haya yanatufundisha pia jinsi gani unaweza kutupia kanuni za kiBiblia katika mazingira ya kila siku.

UPEKEE:

Nini kinachofanya masomo ya stonecroft kuwa wa kipekee sana kuliko masomo mengine ya kiBiblia katika soko la mafundisho ya Biblia?

• Habari njema ya agano jipya: masomo haya yameundwa katika mtindo wa kutumia agano jipya kwa sababu kurasa zimewekwa katika vifungu vile unavyotakiwa kuvitafuta ndani ya Biblia ili kuweka urahisi kwa wasomaji wa masomo haya. Kurasa hizi zilizowekwa katika vifungu hivyo vimetoka katika Biblia ya toleo la 4 good news new testament. na tafsiri hizi zinakubaliwa sana na watu mbalimbali katika madhehebu tofauti tofauti.

• Masomo haya yameandikwa katika kwa mfumo ambao ni rahisi wa kwamba hata Yule ambaye ni mara yake ya kwanza kutumia Biblia basi anaweza kuyatumia vizuri tu. Na haya masomo yanaweza kutafsiriwa kwa urahisi tu sana katika ulimwengu mzima kwa kutumia lugha yeyote ile.

• Kiongozi ni mwezeshaji tu na sio mwalimu wa Biblia.

VIFAA:

Masomo ya stonecroft ya kiBiblia ni rahisi sana kusoma.

Maelezo kwa kiongozi yamefungiwa katika mistari iliyowekewa nukta nukta. Kwa hiyo hayatakiwi kusomwa kwa sauti.

Maelezo mengine yameandikwa yakiwa ndani ya viboksi yapo katika kitabu kile cha kujisomea au cha kusoma. Sehemu hii inatakiwa kusomwa kwa sauti na wale wahisika wenyewe yaani wanafunzi wa mmasomo haya.

Ukionna nukta zimeongozana namna hii (…..) inaonyeshs ya kwamba kiongozi inatakiwa aruhusu kundi ili kuweza kushiriki kwa kujibu maswali, kusma mistari ya Biblia, au kujadili maada husika.

KABLA YA MASOMO :

Vitu vichache vya muhimu:

• Uhakikiwe kuwa wewe ni kiongozi wa stonecroft kwa kukamilisha mchakato wa maombi katika Stonecroft.

• Soma malengo, na maelekezo ya masomo haya husika.

• Pata vifaa mbalimbali utakavyo taka kwa ajili ya masomo yako kutoka katika huduma hii ya Stonecroft _ (800) 525-8627.

• Vifaa vinavyohitajika katika mafunzo haya ni :
a. Vitabu vya kujifunzia
b. Mwongozo
c. Kadi za taarifa

• Tafuta sehemu nzuri kwa ajili ya kujifunzia. Kuwa na muda wa kujifunza ukiwa upo nyumbani, ofisini, kwenye migahawa na katika sehemu mbalimbali.

KUJIANDAA KWA AJILI YA KUJIFUNZA:

• Maliza somo kwa kukamilisha kuandika majibu yako kkatika kitabu chako cha kujifunzia ,kabla ya kusomo mwongozo. Hii itakusaidiakatika kujua na kuelewa mafkirio yaw engine na jinsi ambavyo majibu yako uliyoyajibu yapo.

• Fanya mazoezi ya kusoma kwa sauti kama inawezekana. Pigia mstari maneno na vifungu ambavyo vitakusaidia katika kuelezea mbele ya kundi lako. Kumbuka muda ambao unatakiwa kwa ajili ya kusoma ujumbe wako, hii itakusaidia katika kujua muda gan uliobaki wa majadiliano katika kipindi hicho.

• Thibitisha mahali, muda na ulinzi wa watoto kama kutakuwa na uwezekano wa kufanya hivyo.

• Waombee wote wale ambao watakuwa wakihudhuria katika masomo kujifunza.

WAKATI WA KUJIFUNZA/ WAKATI WA MASOMO:

Gawa vitabu vya kujifunzia na agano jipya na pia kusanya malipo. Kusanya mapato au malipo na rudisha vile vitabu vilivyobaki wakati ulikuwa unagawa.

Anza kipindi kwa maombi. Kukiwa na mtu yeyote anayeuliza, utamruhusu kuwa aandike swali lake nyuma ya kitabu chake sehemu ya maombi (prayer request page) ili iwe kama kumbukumbu yay ale maombi ya katikati ya wiki. Kama swali lililoulizwa linataikiwa kjibiwa kwa wakati huo liambatanishe na kulijibu wakati unaanza kipindi.

Kumbuka kuwa katika kipindi cha awali yaani cha kwanza, kila mtu ataandika majibu katika kitabu chake ha kujifunzia wakati wa kujifunza, au wakati wa masomo. Hamasiha makundi yote kusoma kabla ya kuonana ili kuweka kumbukumbu ya somo hilo.

Soma na uwakilishe taarifa katika kitabu kile cha mwongozo kwa njia ya kujadiliana, hapo ukiwa unawaangalia kwa sana wanafunzi wanachokifanya. Jifunze na soma na makundi yaliyopo; hutakiwi kuwa wewe ndio mjuaji sana wa Biblia.

Kiongozi anaseti toni na kasi ya kujifunza kwa:
• Kuanza na kumaliza kwa wakati uliopangwa.
• Kutumia mwongozo na Biblia kama vitabu vya kurejea. Vifaa vingine havitakiwi ambavyo havina maana yeyote katika kipindi hicho.
• Kuhamasiha kila mtu katika kushiriki katika majadiliano na kuangalia kuwa hakuna mtu anayetawala kundi kwa kuzunumza yeye peke yake.
• Kuweka hisia kwa Yesu Kristo, iswe kisiasa, au kimaandishi, au katika mambo ya kijamii. Kumbuka kuwa mabo ya kisiasa, mambo ya kijamii yote haya yana mazingira yake ya kuweza kuyaelezea.

Mara zote angalia wale ambao wako ndani ya kundi hilo unalowafundisha ambao hao ndio watakuwa viongozi wazuri kwa masomo ya baadae.

Kama kiongozi, kuwa wa mfano kwa wale unaowaangoza. Kataza watu kuzungumza vitu sirini, mbali na kundi lenyewe husika, omba pamoja nao na uwahamasishe katika kutafuta ushauri mzuri wa ki Mungu.

Waulize wahusika wenyewe yaani wanafunzi katika kufikiria ni watu gani ambao wanaweza kuwaalika kwenye masomo mengine. Wahamasishe katika kuwaombea watu wengine kwa majina yao.

VITU MUHIMU VYA KUKUMBUSHA:

Kama huwezi kuongoza masomo kwa sababu yeyote ile, kama kuna mtu anayeweza kufanya hiyo kazi vizuri basi anaweza kufanya hiyo kazi badala yako.

Kwa taarifa zaidi kuhusu taratibu, vifaa, au au jinsi gani uanaweza kuongoza wasiliana nasi kupitia stonecroft bible studies at (800) 525-8627.

“Kesheni, simameni kimara katika imani, fanyeni kiume, mkawe hodari. Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo”
1 Wakorintho 16:13-14


UTANGULIZI
ROHO MTAKATIFU YUKO WAPI?

Watu wengi wanaweza kuzungumzia maisha ya Kikristo katika njia tofauti tofauti, kwamba kuna mambo amabayo ya naweza kubadilika badilika. Wanafurahia muda ule wanapokuwa karibu na Mungu, lakini wanashindwa kujizuia mara zote hasa wakati wa mateso au wakati wanapopitia magumu.

Jonathan Edwards, ambaye anajulikana kuwa ni mwanatheolojia mkubwa sana huko marekani, alisema kuwa, maisha ya mkristo sio mwendelezo wa mawazo yaliyo juu ya mlima. Lakini ni kuishi na uwazi wa Mungu, na uwepo wawake nyumbani, shuleni, katika sehemu za kazi, kanisani, na katika jamii. Ni kuwa na Mungu katika maisha yetu.

Hicho ndicho ambacho masomo haya ya Biblia yanajiusisha nayo. Tunataka kumjua Roho matakatifu katika ma isha yetu kila siku. Juu ya yote, kama ingewezekana kuishi maisha ya Kikristo sisi wenyewe, Munu asingeweza kutupatia Roho Mtakatifu katika maisha yetu. Ni nguvu zake na uwezo wake ambao unaongeza uwezo wa kuwa naye bila tatizo lolote lile.

Hatumtumii Roho Mtakatifu.
Roho Mtakatifu anatutumia sisi.

Roho Mtakatifu yuko wapi? Anaishi na anafanya kazi na pia anaishi ndani ya wale wote wanaomwamini Yesu Kristo. Uendelee kufurahia uwepo wake ndani ya maisha yako.

Lucille Fern Sollenberge.

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

 

 
 
 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us