Project Hope     home >> stonecroft>>roho mtakatifu yuko wapi?>> somo la pili (2)>>la tatu (3)
Stonecroft - Roho Mtakatifu yuko wapi? -La Tatu (#3)
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

SOMO LA TATU (3)
ROHO MTAKATIFU ANAWEZA KUNISAIDIA KUKUA?

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #3 Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #3

LENGO LA SOMO
• Kujifunza zaidi kuhusu ulinzi na uwezo war oho Mtakatifu ndani ya maisha yetu.
• Kuanzisha mipango binafsi na maombia binafsi na kujifunza Biblia.
• Kutambua uhuru kutoka katika himaya ya dhambia kwa nguvu ya Roho Mtakatifu ndani ya maisha yetu.

MAOMBI
Baba uliye juu mbinguni, tunatambua kuwa siku zote hatuna nguvu ya kushindana na dhambi katika maisha yetu. mara zote hatufanyi kama vile wewe unavyotaka kama watoto wako kufanya. tusaidie sisi kujua vitu mbali mbali ambavyovitatusababisha kuwa tofauti katika maisha yetu. tunaoma katika jina la Yesu Kristo …….AMEN

MAONI YA KIONGOZI
Maeleze ya kina kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu yapo katika Yohana 14 -16. Sura hizi tatu ni mambo ambayo Yesu alikuwa akiwaambia wanafunzi wake kabla hajaenda katika bustani ambako ndiko aliko kamatwa. Hizi sura ndizo tutakazososma katika wiki hii ya ya kujisomea au kujifunza.

Watie moyo wana kikundi ili wataje mstari wa biblia walio uchagua.

KUJISOMEA BIBLIA KWA JUMA

(Use your Bible or Africa Bible Verse Handbook)

Soma vifungu vya Biblia hivi hapa chini na uweze kukopi mistari a,mbayo unafikiri ni ya muhimu sana katika kusoma.

Yohana 14:1-14
Yohana 14:15-31
Yohana 15:1-17
Yohana 15:18-27
Yohana 16:1-15
Yohana 16:16-33

Kitu cha kushangaza tulichokisoma kutoka katika masomo yetu kuhusu Roho Mtakatifu ni anaitwa Mungu, a na sifa za Mungu, na anafanya kazi anazofanya Mungu.

Wiki iliyopita, tulijifunza kuwa Roho Mtakatifu anahusika katika kuzaliwa kwetu ndani ya familia ya Mungu.

Ni kitu gani ambacho Roho Mtakatifu anafanya ili kutudsaidia sisi kujua kuwa tunahitaji msaada baada ya kuokoka?.........(Roho Mtakatifu anachukua hatia ya dhambi zetu kabla hatujaokolewa Yohana 16:8.)

Je anajishughulisha vipi na sisis baada ya kuwa Wakristo?........(Anaingia ndani ya maisha yetu pale tunapomwamini yeye kama mkombozi wetu na kuanza mafundisho yake na kazi ya kutulinda Yohana 16:13.)

Tunapompokea Yesu Kristo kama bwana na mwokozi wetu, tunakuwa tayari tumepewa uhakika wa maisha ya milele na Mungu. Wokovu haungalii kuishi kwetu vizuri, yaani mkuwa na nyumba nzuri, maisha mazuri N.K lakini kwa kuwa na uhakika kuwa Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi badala yetu hilo tu linatosha. Sisi kama waamini tuehakikishiwa tayari kuingia mbinguni baada ya kufa.

Roho Mtakatifu ni alama tu moja wapo ya kwamba Mungu anatumiliki, na kutufanya kufanya yale Mungu anayoyataka.sisi kama waumini au washirika wake kristo tayari tumesha tiwa muhuri kuwa asisi ni wana wa Mungu na wokovu upo kwetu.

Somo letu la leo linatuonyesha ya kwamba ni jinsi gani Roho Mtakatifu anaishi ndani yetu na jinsi gani anavyotusaidia kuishi maisha ya Kikristo yenye utii.

ROHO MTAKATIFU NDANI YA MAISHA YETU

Sisi kama watu tuliokoka, sio wafungwa tena wa dhambi. Shetani aliuwa ni Bwana mkatili, lakini sasa Yesu ndiye BWANA wetu mpya na anatupenda sana sisi.
Kwa sasa tuko tofauti na tunajua ni jinsi gani ambavyo tunaweza kuishi maisha ya kiMungu.
Je unajuwa rasilimali hizo tulizonazo ni zipi?...... ( Uwepo war oho Mtakatifu, ulinzi wake, neno la Mungu, na maombi.)

Maisha yetu ya Kikristo yanakuwa pale tunapoendelea kumtii Roho Mtakatifu. Anatusaidia kuachana na tabia mbaya, anatusaidia kuelewa Biblia, na kujifunza jinsi ya kuomba. Maisha ya Kikristo ni maisha ambayo kila siku inakuwa ni kukua ambayo yanaanza pale ambapo Roho Mtakatifu anaingia ndani yetu. Kuna mida mingi sana ya majaribu, kutokutii na uasi. Kwa kuwa Roho wa munu yu ndai yetu anaendela kutusaidia kuendelea kukua katika kimo kingine.

1. Nini annachokifanya Roho Mtakatifu kwetu, kutusaidia ili kukua kiroho?
a. 1 Yohana 2:27……. (Atatufundisha.)
b. Yohana 16:13-14…… (Sikiliza vitu hivi viwili.)
(1. Ataonyesha au atafunua ukweli kuhusu Mungu.)
(2. Ataleta utukufu kwa kristo, sio kujitangaza yeye kama yeye.)
c. Warumi 8:14..…(Roho ya Mungu itakuongoza).
d. Wagalatia 5:22-23..… (Atazalisha matunda yake katika maisha yetu.)
e. Matenndo ya mitume 1:8…. (Anatupatia nguvu ili tuweze kumtambua yeye.)

Kazi ya roo Mtakatifu ni kutufanya sisi, kama kristo kwa kutufundisha, kufunua ukweli,kumtukuza kristo, kutuongoza, kuzaisha matunda na kutupatia nguvu ili kuwa na nguvu ya kuweza kumtambua yeye na kumhisi.

MAOMBI

Maombi ni nguzo muhimu sana katika kutaka kuwa kama kristo. Je maombi ya kriso yalikuwaje?..........mstari ambao unatupa au unatukumbusha kuwa maisha ya kristo yalikua ya maombi sana upo katika ukurasa wa 90, ma rko 1:35.
Kama mwanadamu, Yesu alijua kabisa kuwa kuna muda ambao alitakiwa kuwasiliana na baba, kuzungumza naye, kutafuta mapenzi yake na na Baraka zake.

1. Je, Roho Mtakatifu anatusaidiaje sisi kuomba?
Warumi 8:26…... (Anatusaidia katika madhaifu yetu ,na anatuombea sana sisi kwa yale mambo hatuwezi kuyapeleka)

Mungu aliumba wau ili awe na ushirika pamoja naye. Alituumba sisi kwa mfano wake ili kwamba tuwe na uwezo wa kumwelewa na kumfurahia yeye. Tunazungumza na Mungu kwa njia ya maombi. Anaongea na sisi kwa kupitia kitabu alichokiandika ambacho ni Biblia.
Soma 1 Yohana 5:14-15…..

Muda mwingine Wakristo hawaombi kisawasawa, wanabakia kusema tu maombi. Maombi yetu thabiti yanatoka ndani ya mioyo yetu. Kwa hiyo yanaunganisha ya moyo wa Mungu, ambaye anawasiliana na sisi kupitia Roho wake Mtakatifu. Kwa kuwa Yesu amtupa uhuru wa wa kuomba kwa Baba kwa jina lake, tunaomba na Mungu anatujibu, kwa sababu tunaomba kwa mapenzii yake.

3. a. Mungu alituambia nini sisis kuhusu muda gani au wakati gani tunaotakiwa kuomba?
Ukursa 523, 1 Wathethalonike 5:17……..(Omba kila mara na kila wakati)

b. Ni sifa gani ya Mungu ambayo inatufanya sisi kuomba kila mara na sehemu yeyote?..........(Yeye yupo sehemu yeyoteile na muda wote, yupo kila mahali)

4. a. Mungu alisema nini kuhusu maombi katika Mathayo 6:5-6?..........
(Usifanye kama maonesho katika maisha yako, unaweza kuomba peke yako ukiwa katika chumba chako na Mungu wako)

b. Nini alichokisema daudi kwamba angezungmza na Mungu? Zaburi 55:17……
(Asubuhi, mchana,na jioni)

c. Kama una muda wa mara kwa mara wa kuomba kila siku, anzisha sasa . Andika plani yako ya maombi ya kila siku kama ulikuwa hufanyi hivyo.

KUOMA BIBLIA

Kama Wakristo tuna faida kubwa sana ambayo haikuwepo tangu hapo awali kabla hatujawa Wakristo. Roho Mtakatifu anatufundisha na anatusaidia kuelewa nini Biblia inasema. Soma 1 Wakorintho 1:18…….. Wengi wetu tulikuwa hatuelewi Biblia kabla hatujawa Wakristo. Je unahisi tofauti yeyote na kipindi ambapo ulikuwa hujapata msaada huu war oho Mtakatifu?......

5. Kukua katika Ukristo inatakiwa tuanzishe ratiba ya mara kwa mara ya kusoma Biblia. Tafuta muda ambao wewe unaona kuwa wewe utakufaa katika kukamilish a hili……………

Itakuwa ni vizuri hata ukiwa unaamka mapema au unachelewa kulala kwa ajili ya kusoma Biblia na kuomba kwa manuafaa yako na maisha yako kiujumla. Lakini kuwa na ushirika na Mungu kila mara ni kitu cha muhimu sana katika maisha ya kila siku ya muumini hasa pale unapokuwa unakuwa katika maisha ya Kikristo, kama vile rho mtgakatifu navyo tufundisha sisi kwa kupitia neno la Mungu.

Kuwa na ushirika na Mungu ni kitu kinachofanya maisha yetu ya Kikristo kama kujua utatu ndani ya ma isha ya Kikristo. Kwa kupitia maombi, na vile Mungu a navyotupa kupitia umakini wetu tunaposoma neno, tunafikia hatua ya kuelewa kuwa Mungu ndiye anayeyaa ngalia maisha yetu. Kuishi chini ya ulinzi war oho Mtakatifu inamaanisha kuwa sisi tunaishi na kukua katika uhusiano mzuri na kristo.
UTII

6. Ni ushauri gani ambao Mungu anatupa kuhusu kusoma Biblia? Yakobo 1:22-25…..
(Tii kile unachokisoma, na kifanyie mazoezi).

Tunapotii kile tunachokisoma katika neno la Mungu, tunaweza kuzuia kufanya maamuzi ambayo sio sahihi, na utabarikiwa sana na Mungu.

Utii kwa munu ndio utakao tuwezesha sisi kukua kama Wakristo. Maarifa ya neno la Mungu ni muhimu sana, lakini kujua bilia na kutokuitii ni hatari sana.

Roho Mtakatifu anachukua dhambi zetu au hatia yetu katika maisha yetu kabla hatujawa Wakristo. Na bado anaendfelea kuchukua hatia yetu na kutukumbusha kutokutenda vibaya, kuwa na mawazo potofu, kuwa na mitazamo mibaya ,ambapo haya yote yanatusababisha sisi kutokukua kiroho.

Soma Wagalatia 5:17…..
Ukweli ni kuwa hatuwezi kutii mapenzi ya Mungu kwa nguvu zetu sisi wenyewe. Tunamhitaji Roho Mtakatifu kutupatia nguvu na uwezo wa kufanya hivyo.

Kama Wakristo tunajaribiwa kwa kufanya vitu kwa njia zetu wenyewe bila kumshirikisha Roho Mtakatifu kama kiongozi wetu. Sisi tuna panga sisi wenyewe kukupambana na majaribu ambapo kwa wakati mwingine inaonekana ni njia nzuri sana ya kuweza kupambana na majaribu. Lakini Mungu anatuia moyo kuwa kukaa nay eye itasaidia zaidi kuliko kuaa peke yestu kwa atatusadia katika kusimama imara katika mambo tofauti tofauti, hata ikiwa ni katika majaribu atatusaidia. Yeye ametupa ahadi kuhusu hili, soma 1 Wakorinntho 10:13……. Huu mstari ni vizuri kukariri. Andika hapa

7. je inawezekanaje kwetu sisi kumhuzunisha Roho Mtakatifu?.
Waefeso 4:25-32……… (Roho Mtakatifu anahuzunika pale tunaposhindwa kumtiii yeye)

Tunapo sema uongo, unapokuwa na hasira, tunapowafanyia watu wengine mabaya, kuwa na machukizo, au kuwa na mioo migumu, tunamkasirisha Roho Mtakatifu. Hii, inatika kwa sababu hatujali maonuyo yake. Kwa hiyo ili sisi tuweze kukua inatakiwa haya mambo yote tuachane nayo ili tuweze kukua kiroho.

Soma Waefeso 4:30 tena.. Huu mstari unaodhihilrisha ukweli mwingine. Kukaa kwa Roho Mtakatifu ndani yetu ni ishara ya kwamba Mungu a natumiliki sisi. Sisi hatuko peke yetu. Tumenunuliwa kwa ,gharama kubwa sana. Soma 1 Wakorintho 6:19-20...

8. Umeumbwa ili kumtukuza Mungu. Kazi kubwa ya Roho Mtakatifu ni kuhakikisha kuwa anakusaidia katika kuishi maissha ya kuweza kumtukuza Mungu.

a. oredhesha baadhi ya maeneo ambapo Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani ya maisha yako ili kukufanya wewe kama kristo……..

b. orodhesha maeneo ndani ya maisha yako ambayo Mungu tayari ameshakupatia ushindi………..

Wagalatia 5:16…………

Wakati Roho Mtakatifu anadhibiti maisha yetu, badala yetu sisi wenyewe, anatufanya kuwa kama kristo.

U funguo wa kuweza kubaki na kuwa kama Yesu ni kukazana kusoma neno la Mungu yaani Biblia na kuweka muda juu ya Mungu kwa maombi sana. Tunapotaka au tunapounda urafiki na watu mara nyingi tunakaa pamoja, hivyo basi inatakiwa hata kwa upande wetu tufanye hivo kuwa na urafiki wa karibu na Mungu, kwa kusoma bib lia na kuomba ili tujue anasema nini kuhusu sisi. Roho Mtakatifu atakuwa mwaminifu katika kutufundisha sisi, endapo tukiwa wakrimu na kufanya kwa nafasi yetu kile kinachotakiwa kufanywa kwa matakwa yake, na kwa kumsikiliza na kumtii Mungu.

Maombi ni mrejesho wa kile ambacho Mungu amesema. Kila asubuhi tunaweza kuomba kuhusu kazi zetu, kumuomba Mungu kufunua mipango yake kwa ajili yetu juu ya siku husika. Tunaweza kumuomba yeye kutupa hekima ili tuweze kukamilsha vitu katika njia ya kumpendeza Mungu.

Unapoishi ndani ya uwepo wa Mungu kila mara, maisha yetu yatabadilika na kuwa na maana mpya sana. Kila siku tutaona ukuu wa Mungu ukiwa unafanya kazi ndani yetu.

9. Fikiria majibu yako katika swali la 8 na andika maombi yako ya kumshukuru Mungu kwa maendeleo ambayo unayaona ndani ya maisha yako………..

MAOMBI

Baba yetu, asante kwa kutupatia Roho Mtakatifu wa kutufundisha sisi na kutusaidia kuelewa ukweli wa neno lake. hamu ya mioyo yetu ni kukutii wewe. asante kwa kutusaidia katika kukua tunapokuheshimu wewe. katika jina la Yesu Kristo…..AMEN…..

 
 

 

This is a translation of 'Who is the Holy Spirit?' Stonecroft's Guide Book Lesson #3 in Swahili, the English version of Who is the Holy Spirit? is available online from Stonecroft's website.

This transforming study will reveal who Jesus is, what He does, and what life is like when He lives within you. Learn what the Holy Spirit does in the life of a Christian and how He can help you grow to be more like Christ. (6 lessons)

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #3 Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #3

Download Swahili Lesson #3 Student Study Book

 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us