Project Hope     home >> stonecroft>>roho mtakatifu yuko wapi?>> la nne (4)>>la tano (5)
Stonecroft - Roho Mtakatifu yuko wapi? - La Tano (#5)
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

SOMO LA TANO (5)
KUISHI KATIKA NGUVU YA ROHO MTAKATIFU

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #5 Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #5

LENGO LA SOMO
• Kuhjifunza umuhimu na kuruhusu Roho Mtakatifu kuwa ndani yetu.
• Kutambua kuwa maisha ya ushindi ya mkrishto yanatokana na Roho wa Mungu kuwa ndani yetu.
• Kuelewa kwa nini utii na uzao ni muhimu sana katika kujazwa kwa Roho Mtakatifu.

Kwa sababu ya utata uliopo ndani ya hili somo, itakuwa vizuri kurudia mwongozo unaotuongoza katika mafunzo haya. Kama majibu yaliyotolewa yana kinzana kwa kukubali majibu kwa kutolea ufafanuzi hata kidogo basi unaweza ukaendelea na somo. Kama mtu "akizungumzia kunena kwa lugha"unaweza ukasema kuwa,“ kwa sababu makanisa yanatofautiana katika mafundisho juu ya hili, lakini ngoja nikupe kifungu ambacho kinajibu swali lako . Tafuta muda ukasome katika 1 Wakorintho 14:1-40 utakapo kuwa nyumbani"

MAOMBI
Baba uliyejuu mbinguni, asante kwa kutupa neema ya kuishi maisha ya Kikristo. Tufundishe sisi umuhimu wa kukutii wewe. Katika jina la Yesu, AMEN

MAONI YA KIONGOZI
Unaweza ukawa umegundua kuwa kuna vifungu vingine ndani ya masomo haya yaliyopita vimekuwa vikijirudia.Lakini ni kwamba vifungu vya Biblia vikijirudia katika kusomwa haina tatizo bali tutakuwa tunaongeza ufahamu juu yay ale tuyamayo.


KUJISOMEA BIBLIA KWA JUMA

(Use your Bible or Africa Bible Verse Handbook)

Andika rejea ya mstari ambao umekusaidia wewe kwa umuhimu mkubw asana katika vifungu vifuatavyo.

Wagalatia 5:16-26
Warumi 6:1-11
Warumi 6:12-19
Warumi 6:20-23
Warumi 8:1-8
Warumi 8:9-17

Uwepo war oho Mtakatifu ndani ya maisha yetu na zawadi au vipawa anavyo tupatia, vinatufanya sisi kuwa kama Wakristo ambao tunafanana na kristo mwenyewe. Kama waamini, tunaye Roho Mtakatifu kila mara ambaye anayetulinda kila mara, anatufundisha, na kutupatia nguvu ya kuweza kushinda katika hali mbalimbali. Kwa kuwa Roho yupo kwa ajili yetu na kufanya kazi kwa ajili yetu basi tutakua tunaona ushindi mara kwa mara.

1. Kukaa kwa Roho Mtakatifu ndani yako kumekusaidiaje ndani ya wiki hii? .......
(Waruhusu watu kushirikiana majibu yao watakayo toa.)


Mwandishi Charles Swindoll alitoa msaada juu ya ufafanuzi war oho Mtakatifu ndani ya maisha yetu.

Alizungumzia kuhusiana na kijana mdogo amabye jina lake alikua mtenda Dhambi, ambaye alipokea gari kkutoka kwa baba yake, lilikuwa gari jekundu na lilikuwa linaitwa Wokovu. Lilikuwa ni gari jipya na zuri sana. Muda mwingi Yule kijana alikuwa anawaeleza watu wengi kuwa amepata zawadimkutoka kwa baba yake, alikuwa hatarajii kuwa na gari kama lile, na asingeweza kulilipia, yaani hiyo ilikuwa ni zawadi tu ya moja kwa moja kutoka kwa baba yake.

Hili gari lilimfanya yeye kubadilika na kuwa na furaha sana, a mbapo likabadili hata jina lake kutoka mtenda Dhambi mpaka jina la Kuokolewa.

Baadae, alionekana akisukuma lile gari lake chini ya njia kuu, mtu mmoja jina lake alikuwa anaitwa Msaada, alikuwa akitembea alijitambulisha yeye mwenyewe, na kumuuliza yula kijana kama angetaka msaada wowote.

Tle kijana akamwambia “hapana asante sana nashukuru “ Aliyeokolewa akajibu
“Umesukuma gari lako tokea mbali?” Msaada akauliza.

“Kama maili 200 hivi.Imekuwa inaniwia vigumu, lakini hii yote nafanya kwa sababu baba alinipatia hili gari.” Aliyeokolewa akajibu

Msaada akasema, “Niruhusu mimi nikusaidie, kuna kitu ambacho wewe hukielewi”.
Msaada akafungua mlango wa gari, na yule kijana akashtuka kidogo, kw ahiyo Yule msaada akaingia ndani ya gari, kwani tangu Yule kijana alipopewa lile gari alikuwa amelipumzisha tu.

Msaada akazunguka kwa upande mwingine, na akakaa katika kiti cha dereva, na akawasha gari ambapo likaanza kutembea mara wakaingia barabarani na kuanza kuondoka vizuri kabisa bila tatizo lolote.

Kwa hiyo Yule kijana akakaa pale kwenye gari akiwa anashangaa.Alikuwa akimruhusu sasa hata Yule aliyetoa Msaada kufanya kile ambacho hakutaka hata kukifanya. Alifikiri kuwa kufika mwisho wa ile barabara ilikuwa nndio mwisho wa majukumu yaka. Alitabasamu saana, na akagundua Yule kijana kuwa tangu amepata ile zawadi kutoka kwa baba yake ile ilikuwa ndio tabasamu lake la kwanza tangu kupokea ile zawadi.

Hiyo ni picha halisi ya Wakristo wengi.tunajua kabisa kuwa kulikua hakuna njia ambayo tungeweza kulipa kwa ajili ya wokovu huu. Hii ilikuwa ni zawadi tu, lakini pia hatujui kuwa nguvu yenyewe ya kuishi maisha ya Kikristo pia ni zawadi.

Swindoll alihitimisha kwa kusema “ mtu aliyekupa gari, alikupa na dereva. Anaweza kumiliki vizuri tu. Unapotaka kutoa tairi juu ya mikono yake weqe utakuwa una matatizo”.

Ili kuendelea kuishi katika maisha mazuri ya Kikristo ni kuw ana Roho Mtakatifu, anapoishi ndani yetu na kupitia wewe.

Kua wakati ni vigumu san kukubaliana na ukweli kuwa, tunaweza tusifanye kitu chochote, ili kufanya wokovu wetu ukawa imara zaidi kuliko siku ile ambayo tulipmpokea Yesu kama mkombozi wetu. Tunataka kufanya kitu kwa aji.li ya Mungu., lakini badala yake Mungu alifanya hicho kwa ajili yetu. Wokovu ni zawadi ya upendelea ambayo haina malipo yeyote, kwa hiyo ni maisha yetu mapya.

Kifo cha Yesu Kristo pale msalabani, kilileta zawadi kwetu sisi ya wokovu, lakini ni ufufuo wake, ambao ulileta nuvu zaidi kuishi katika maisha ya utii. Soma katika Warumi 5:8-10……

Kuokolewa kwa kifo cha Yesu Kristo, lakini nguvu ya kuishi ni ufufuo wake.


2. Kifo cha Yesu kilikuokoa wewe, je ufufuo wake umekufanyia nin I wewe?

Waefeso 1:18-20…………

2 Wakorintho 13:4………..
(Unatupatia sisi nguvu ya kuishi vile Mungu anavyotaka sisi tuendelee kuishi).


Masiha yetu ya kila sisku na shughuli za kila wakati zote zinatolewa kwa sanbabu ya kufufuka kwa Yesu Kristo. Tunakubali na kupokea zawadi ya wokovu kwa imani. Pia tunaishi maisha ya Kikristo kwa imani.


Hatuwezi kuishi maisha ya Kikristo kwa nguvu zetu wenyewe. Ni kwa nguvu ya Mungu pekee ambapo tunaweza kuishi na kutii kile ambacho Mungu ametruagiza kwa mapenzi yake. Nguvu ya Roho Mtakatifu katika maisha yetu inatakiwa iwe ni ya kumtumikia Mungu na watu wengine. Haitakiwi kutumika kama faida yetu sisi wenyewe. Tumejazwa na Roho Mtakatifu, kwa hiyo tuna uwezo wa kuishi kama vile Mungu alivypanga mipango yake kwetu sisi.

Soma katika Waefeso 2:10…………


Sisi kama sisi,hatuwezi kufanya kile kitu ambacho Mungu amekipanga.hiyo itakuwa kama kusukuma gari, usije ukajichanganya. Tunatakiwa pia tuendelee kutoa nguvu ya kumalizia kazi , lakini inafanywa chini ya uangalizi wa roho.

Wakristo wamepokea Roho Mtakatifu (Warumi 8:9-10). Sasa kwa nini Biblia inatuambia kuwa tujazwe na Roho Mtakatifu?

Kujjazwa na Roho haimaanishi kuwa inatakiwa kupata kile kitu ambacho hatunacho. Inamaanisha kuwa sisi kama sisi inatakiwa tujazwe na Roho Mtakatifu.
Tujishushe kwake kjila mara. Ili kufanya hili, tujishushe sana kwake nan a sio kujikontrol sisi wenyewe. Tunatakiwa tuache saizi ,kusukuma gari letu la kiroho, badala yake tunatakiwa kutii na kufurahia mahala ,popote pale ambapo Roho Mtakatifu atatuongoza.
Soma Waefeso 5:18….. kwa nini unatakiwa kujazwa na Roho wa Mungu inafananishwa na kulewa ?.........(Kwa sababu Matendo yestu yanasukumwa na Yule .mtu anaye ishi ndani yetu.)

Watu wakiwa wamelewa, wanakuwa wako cini ya utawala wa pombe waliyoinywa. Kwa njia hiyo hiyo, Wakristo ambao wamejazwa na Roho Mtakatifu, wana uwezo wa kufanya vitu katika njia ya Mungu, na sio katika njia tuzitakazo sisi wenyewe.


3. Elezea mtu ambaye amejazwa na Roho Mtakatifu. Waefeso 5:18-20……
(Mtu ambaye amejazwa na Roho Mtakatifu, anajishusha chini ya ugtawala war oho Mtakatifu, kuongea kwa lugha ya kristo kwa watu wengine, kuimba nyimbo za kumtukuza Mungu, na kumpa shukrani kwa kila kitu).

Mungu anatulazimisha sisi kujazwa na Roho Mtakatifu sababu kuu mbili: ili kukua na kumtumikia Mungu katika njia nzuri zaidi.

Mmkristo mpya anapewa Roho Mtakatifu, lakini hiyo ,haimaanishi kuwa tayari kakua kiroho. Kukua kiRoho kunakuja pale anapojazwa na kuishi maisha ya utii kwa muda mrefu tu.
Wakristo wa korintho hakua wamekua, Biblia inasema na inaeleza kwa uzuri kabisa kuwa kwa nini hawakuwa wamekua ilikuwa na kwa sababu ya uchanga wao. Soma katika Wakorintho 3:1-3……..

Tumejazwa na Roho Mtakatifu ili kuweza kukamilisha kazi ambayo Mungu ametupatia sisi. Soma Matendo 9:17 na 20……… Paulo alijazwa na Roho ili kukamilisha kazi ambayo alipewa na Mungu na vile Mungu alivyokuwa amepanga juu ya kazi yake.

Tunapompokea Yesu Kristo kama mkombozi wetu, Roho Mtakatifu anakuja ndani yetu, hakuna masharti ya kumpokea Roho wa Mungu. Lakini kuna masharti ya kujazwa na Roho Mtakaytifu, ambapo inatakiwa tumtii sana Mungu ndipo tutajazwa na Roho Mtakatifu.

4. Ni masharti gani ambayo yameainishwa katika kumtii Roho Mtakatifu?

Warumi 6:19…….. (Achilia maisha yako chini ya Mungu baba)
Warumi 12:1…….. (Imejikita katika kumtumikia Mungu)
1 Petro 4:19……… (Kutii, hata kama itaonekana kuna mateso. Amini kile Mungu anachokisema; mtegemee Mungu peke yake)


Kuna wakati mwingine sisi kama Wakristo tunatakiwa kujishusha katika utawala wa Mungu. Kujishusha kwetu kunatakiwa kuwe hivyo kwa Mungu wetu mara kwa mara. Tunatakiwa kumwambia Mungu au kumwoma Mungu kubadilisha maisha yetu. Soma katika Warumi 12:2….

Mungu anatubadilisha sisi kutoka ndani, anasafisha fahamu zetu ili kutufanya kufikiri tofaiti na watu wengine. Tunapokuwa karibu na Mungu, tunajipeleka ili kwamab yeye atutumie sisi apendavyo.

Kwa sababu Roho Mtakatifu anamtii Mungu baba, lakini mioyo yetu inataka sana kufanya mambo yenyewe bila msaada wowote ule, kwa kuwa kuna mgogoro wa ndani. Lakini tunapo mruhusu Roho Mtakatifu kutusaidia sisi kujishusha kwa Mungu, ina maana tunachagua kuwa Mungu afanye mambo yote kwa niaba yetu.

Tunapomtegemea Mungu peke tunafanya kile ambacho Mungu anataka sisi tufanye, kuliko kile tunachotaka kufanya sisi kama sisi. Biblia inatuambia sisi kuhusu hili katika Warumi 8:1-5…..

Tunapokua katika kujishusha chini ya mamlaka ya Mungu, tunakua watii, amabapo hii inatusaidia kujazwa na Roho yake.

5. Ni maeneo gani muhimu katika maisha yako yanahitaji wewe kujazwa na Roho wa Mungu ili kukamilisha matokeo yanayotakiwa?............ (Hakikisha kila mmoja anatoa jibu lake)

6. Elezea ukweli kuhusu Roho wa Mungu katika maisha yako katika mitazamo na majukumu/ kazi yafuatayo.

Ushahidi kuwa umejazwa na Roho ya Mungu

Napanga nini pale ambapo mabadiliko yanatakiwa

Kujua kuwa nimeokolewa

Kuwa na muda wa maombi kila mara

Kusoma Biblia mara kwa mara

Kushinda tabia zinazoleta dhambi

Kuwapenda waumini wengine

Kuwa na mitazamo na wasioamini

Hatuwezi kuishi maisha yay a mutii kw anguvu zetu wenyewe bila kupata msaada wowote kutoka kwa Mungu. Tunataka nguvu ya ziada ya kutusaidia sisi. Na ndio maana tukapewa zawadi ya Roho Mtakatifu. Tukifuata utawala wake nasi tutaweza kuishi maisha ya kumpendeza sana Mungu.

Matokeo ya somo hili, jiulize mwenyewe swali hili. Je, nimefikia wapi katika kukaa na Roho Mtakatifu?

Gharama ni kujitoa
Sharti ni utii.
Roho mtakatifu alipoingia katika maisha yangu
Nilimpokea yeye katika utimilifu wake.
Kujazwa na Roho mtakatifu,
Ananiohitaji katika ukamilifu wangu.


7. Andika maombi yako, ambapo ukionesha jinsi ulivyo na hamu ya kuweza kujazwa na Roho ya Mungu.

Kwa kuwa maombi katika somo la 7 ni maombi binafsi,sio muhimu wao kulisema labda wakipenda kufanya hivyo.

MAOMBI

Baba yetu uliye mbinguni tunakushukuru kwa wema wako, na kutufanya kuwa katika mahusiano mazuri na wewe. Asante kwa kutupa nguvu ya kuishi maisha yenye kukupendeza wewe na kushi chini ya utawala wako, tunataka kuwa wako kabisa. Katika jina la Yesu Kristo. AMEN

 

 
 

 

This is a translation of 'Who is the Holy Spirit?' Stonecroft's Guide Book Lesson #5 in Swahili, the English version of Who is the Holy Spirit? is available online from Stonecroft's website.

This transforming study will reveal who Jesus is, what He does, and what life is like when He lives within you. Learn what the Holy Spirit does in the life of a Christian and how He can help you grow to be more like Christ. (6 lessons)

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #5 Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #5

Download Swahili Lesson #5 Student Study Book

 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us