Project Hope     home >> stonecroft>>roho mtakatifu yuko wapi?>>somo la kwanza (1)>> somo la pili (2)
Stonecroft - Roho Mtakatifu yuko wapi? - Somo la pili (#2)
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

SOMO LA PILI (2)
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU NI ZIPI?

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #2 Swahili Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #2

LENGO LA SOMO
• Kujifunza je agano la kale linasema nini kuhusukuhusu Roho Mtakatifu.
• Kujifunza kazi za Roho Mtakatifu ndani ya maisha ya mkristo.
• Kujifunza kuhusu Roho Mtakatifu sehemu ambazo ziliandikwa ndani ya Biblia.
• Kukubali ulinzi na uwezo war oho Mtakatifu ndani ya maisha yetu.

MAOMBI
Mungu mwenyezi, asante kwa kutupatia Roho Mtakatifu wakati tunaokoka. Fungua macho yetu ili tuweze kuona jinsi gani ambavyo anatusaidia sisi. Tunaomba katika jina la Yesu…………AMEN………

Anza somo kwa kuwashirikisha watu katika kusoma mistari ya Kibibilia amabyo waliweza kuichagua katika wiki iliyopita.

KUJISOMEA BIBLIA KWA JUMA

(Use your Bible or Africa Bible Verse Handbook)

Soma mistari ya Biblia ifuatayo na uchague ni mistari mingapi ambayo unafikiri ni ya muhimu sana kwako katika kila mstari unaousoma.

Yohana 3:1-13
Yohana 3:14-21
Matendo ya mitume 1:1-11
Matendo ya mitume 2:1-13
Matendo ya mitume 2:14-21
Matendo ya miitume 2:36-42

MAONI YA KIONGOZI

Tume,kuwa tukijifunza kuhusu maajabu na uhamasisho wa Mungu baba, Mungu mwana na Mungu Roho Mtakatifu. Ni Mungu mmoja tu ambaye anajifunuua kwetu kwa kupitia njia hizi tatu.

Katika somo la kwanza, tulijifunza kuwa Roho Mtakatifualichukua hatia zetu sana kuhusu dhambi zetu na kutusaidia kupata huu wokovu. Kujua Roho ya Mungu, tunahitaji kuwa na ufahamu wa ziada sio mhuu tu ambao tunao ili kuelewa kuwa Mungu yupo na kuwa Yesu alikufa kwa ajili yetu. Tunatakiwa kumpokea Yesu kama mwokozi wetu. Tunapomkubali yeye, Mungu yeye anatupatia Roho Mtakatifu.

Katika muda uliopita, Warumi 8:16 inakuwa kweli katika maisha yetu………….
Tunapomkubali Yesu Kristo kama mwokozi wetu, tunakuwa watoto wa Mungu. Roho ya Mungu iliyoko ndani yetu inaanza kubadilisa maisha yetu ili kufanana na Yesu au ili kuwa kama Yesu.

ROHO YA MUNGU KATIKA AGANO LA KALE

Tunaona Roho m takatifu katika kitabu cha kwanza katika Biblia yaani kitabu cha Mwanzo.
Tulisoma nini kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu katika swali la kwanza kabisa?

1. Tunatambulishwa Roho Mtakatifu katika mstari wa pili (2) katika agano la kale. Aliitwaje na alifanya nini? Mwanzo 1:2…………

(Roho ya Mungu ilikuwepo na ilikuwa imetawala kila sehemu).

Biblia inasema kuwa Roho wa Mungu alikuwa na mzhango mkubwa sana katika uumbaji wa hii dunia. Isaya 40:12-14……….

2. Watu tofauti tofauti walimtolewa Roho Mtakatifu majina mengi sana ambayo yanafunua kazi yake ndani ya maisha yetu pia.

Baada ya kila mstari, andika jina ambalo alipewa Roho Mtakatifu na uoneshe kazi aliyoifanya :

a. Ayubu 33:4…..
Jina: (Roho wa Mungu)
Kazi: (Aliumba watu wote)

b. Ezekieli 36:27……
Jina: (Roho yangu)
Kazi: (Inasaidia watu kuweza kumtii Mungu)

c. Mika 3:8……
Jina: (Roho wa Bwana)
Kazi: (Anatoa nguvu kwa watu ili kuweza kufikisha ujumbe wa Mungu kwa watu wengine)

d. 2 Samweli 23:2…..
Jina: (Roho wa Bwana)
Kazi: (Anaongea kupitia watu. Mstari huu unasema kuwa alisema na daudi, ambaye aliandika Zaburi kwa asilimia kubwa ndani ya Biblia)

Ili kurudia, sikiliza tena kuwa kazi ya Roho Mtakatifu katika agano la kale ilikuwaje. Roho Mtakatifu aliumba watu wote, aliwapa uwezo wa wao kumtii Mungu, aliwapa watu nguvu ya kusambaza ujumbe wa Mungu, na aliongea kupitia mtu binafsi.

Agano la kale linafunua zaidi kuhusu Roho Mtakatifu. Anaitwa Roho ya Bwana, na Roho ya rehema, na Roho ya dua. Majukumu mmengi ya Roho Mtakatifu yapo katika agano la kale. Soma Isaya 11:2……


ROHO MTAKATIFU KATIKA AGANO LA KALE

Ni Roho wa kweli,
Anafunua ufahamu wa Mungu.


Ni Roho wa utakatifu,
Huonesha usafi na utakatifu wa Mungu.

Ni Roho wa nguvu,
Kuwatia nguvu kwa wale wote walichagua kazi yake.

Ni Roho wa hekima,
Anaonesha utu halisi wa Mungu.

Ni Roho wa ahadi,
Kuonesha mambo yajayo au wakati ujao.


Roho Mtakatifu aliwajilia watu katika agano la kale, na kuwatia nguvu watu hao kwa kazi aliyokuwa Mungu amewapa. Kwa mfano, Mungu aliruhusu Roho Mtakatifu kumsaidia Bezalel, kwa kazi aliyokuwa amepewa na katika hema. Soma kuhusu sifa ambazo Mungu alimpa mtu huyu katika Kutoka 31:3…………

Roho Mtakatifu pia katika agano la kale aliwapa nguvu ya ajabu, uwezo mkubwa wa kuweza kungoza taifa kubwa .

Agano la kale halisemi kuwa Roho Mtakatifu alikuja kukaa ndani ya mtu moja kwa moja. Na ndio maana daudi aliomba kwa kadri ya uwezo wake katika Zaburi 51:11……….. katika nyakati za agano la kale. Mungu alichukua Roho yake kutoka kwa mtu wakati kazi yake ikiwa imeshakwisha. Katika Zaburi 51 inatuambia kuwa kutubu kwa daudi na kwa maombi yake akiomba kuwa Mungu asimtoe Roho wake kutoka kwake.

ROHO MTAKATIFU KATIKA AGANO JIPYA

Ufunuo mkuu kuhusu Roho Mtakatifu ndio umejifunua katika agano jipya.
Kipindi cha agano jipya, Roho Mtakatifu aliendela na kazi aliyokuwa nayo tangu alipokuwa katika agano la kale. Aliongea na watu binafsi, aliwapa ulinzi, na kuwawezesha watu kufanya vitu ambavyo wamembiwa na Mungu kuvifanya. Lakini kwa nyongeza tu, katika nyakati za agano jipya na sasa, Roho Mtakatifu akiingia ndani ya mtu anakaa humu milele yote.
Soma katika Yohana 14:16…..

Kwa sasa ukweli kwamba Roho Mtakatifu anakaa ndani ya watu moja kwa moja (milele), hii ndio tofauti iliyopo kati ya kazi ya Roho Mtakatifu katika agano la kale na kazi ya Roho Mtakatifu katika agano jipya.

Hakuna kazi yeyote ya Roho Mtakatifu ambayo iumerekodiwa katika kipindi cha miaka 400 kati ya kitabu cha mwisho cha agano la kale na kitabu cha kwanza cha agano jipya. Hakukuwa na nabii aliyekuwa akiongea au akinena neno la Mungu.

Lakini, baadae mara rooho Mtakatifu akaanza kazi tena ya huduma , kuandaa kwa kuja kwa Yesu Kristo. Tangu ilipotungwa mimba ya Yesu Kristo na mpaka mwisho wake Roho Mtakatifu ndiye alikuwa akiongoza kazi hii ili kufanikiwa na mpango kutimilika.

ROHO MTAKATIFU KATIKA MAISHA YA KRISTO

3. Agano jipya linaweka wazi kuwa Roho Mtakatifu alikuwa na kazi ya ziada katika maisha ya kristo. Oanisha mistari ifuatayo na kazi za Roho Mtakatifu katika maisha ya kristo.

Luka 4:16-18……
Luka 4:1…..
Warumi 8:11……
Matendo 1:1-2……
Mathayo 1:18-20……

a. Kutungwa kwa mimba ya Yesu ilikuwa ni kwa uwezo war oho Mtakatifu. (Mathayo 1:18-20)
b. Yesu alijazwa na aliongozwa na Roho wa Mungu. (Luka 4:1)
c. Yesu alitiwa mafuta na Roho Mtakatifu ili kuhubiri, kuponya wagonjwa na vipofu na kuokoa, na kuwajali waliodhulumiwa. (Luka 4:16-18)
d. Yesu alifufuliwa kutoka kwa wafu kwa uwezo wa Roho ya Mungu. (Warumi 8:11)
e. Baada ya kufufuka, Yesu aliwafundisha mitume wake kwa uwezo war oho Mtakatifu.
( Matendo 1:1-2)

Mistari hii ya kiBiblia inatuambia kuwa Roho Mtakatifu ana uongozi mkubwa sana katika maisha ya kristo alipokuwa hapa duniani. Ingawa Yesu alikuwa na nguvu ndani yake yeye mwenyewe kwa ajili ya kuikamilisha kazi aliyopewa na Mungu, lakini Yesu aliishi maisha yake hapa duniani kwa msaada war oho Mtakatifu. Aliisi kama mwanadamu na kutuonesha kuwa mipango ya Mungu kwetu ikoje na tuweze kuishi kwa namna gani. Kama Roho ilivyomuongoza Yesu, pia vile vile atatungoza na kutuwezesha kuishi kama Wakristo kama tutamruhusu kuingia ndani yetu.


KAZI YA ROHO MTAKATIFU KATIKA UANDISHI WA BIBLIA

4. Tumembiwa kuwa ni jinsi gani ambavyo Biblia 2 Petro 1:21…..

a. nani aliwaambia watu waliondika Biblia kuwa waandike nini?......... (Roho Mtakatifu)

b. Je, ujumbe ulitokea wapi ?........ (Kwa Mungu)


Roho Mtakatifu alliwaongoza wote walinadiika vitabu ndani ya Biblia. Ona kile alichokizungumza Paulo mwandisha wa kitabu cha Wakorintho, 1 Wakoritjo 2:13…..

Roho Mtakatifu alimfundisha Paulo kitu gani afundishe. Je Roho Mtakatifu alimpa Paulo maneno au mawazo aliyotakiwa kuandika?.......(Roho Mtakatifu alimpa kila neno kuandika).

Nani alimpa Roho Mtakatifu maneno? Jibu linapatikana katika mstari tuliousoma katika swali la 4……….(Mungu).

Hii ndiyo sababu tunaita Biblia kuwa ni neno la Mungu. Roho Mtakatifu alikuwa na waadisha ambao na waume, Mungu alisema.

Biblia ni kitabu pekee ambacho mwandishi yupo muda wowote unapokisoma.
Elezea sentensi hii ina maanisha nini….. (Roho Mtakatifu, mwandishi wa Biblia, wapo muda wote unaposoma Biblia, au Biblia inaposomwa).

ROHO MTAKATIFU NDANI YA MAISHA YETU

5. Kila mstari ufuatao wa Biblia, unaonesha hatua Fulani ya kazi ya Roho Mtakatifu.katika wokovu wetu. Oanisha mistari hii na sentesi sahihi.

Wagalatia 3:27
Warumi 8:15
2 Wakorintho 3:18
1 Wakorintho 3:16-17
Yohana 6:63

a. Mungu ni mpaji wa maisha, Roho anatupa maisha ya kiroho. (Yohana 6:63)…….
b. Roho ya Mungu inayoishi ndani yako, inakwambia kuwa wewe ni m wana wa Mungu. (Warumi 8:15)…….
c. Roho Mtakatifu anakubatiza wewe katika umoja na kristo unapookolewa.
(Wagalatia 3:27)……..
d. Roho wa Mungu anayeishi ndani yako anakufanya wewe kuwa hekalu la Mungu.
(1 Wakorintho 3:16-17)…..
e. Roho wa Bwana anabadilisha maisha yetu ili kuonesha utukufu wa Mungu.
(2 Wakorintho 3:18)……..

6. Cagua aliyeyote ile ndani ya maisha yako ambayo unahitaji ulinzi war oho Mtakatifu. Eleza mahitaji yako, na kasha andika maombi yako ukimuomba Roho wa Mungu kukupatia ulinzi unaoutaka katika eneo hilo ulitakalo katika maisha yako………

Chagua mtu ambaye atasema ombi lake mbele ya kundi ili kundi la mjadala liwe la kuwajibika,baada ya maombi,buni na andika maombi yako mwenyewe au au tumia haya yafuatayo katika kuhitimisha.

MAOMBI

Baba yetiu uliye juu mbinguni, asante kwa kutuipatia Roho wako Mtakatifu, ambaye anatupaia nguvu, uwezo wa kufanya yale wewe uyatakayo. Tusaidie tuweze kutambua sauti yake pale anapoongea na sisi katika kujibu maombi yetu. Tunataka kuishi maisha ambayo yanakufurahisha wewe Mungu. Katia jina la Yesu…………

AMEN

 
 

 

This is a translation of 'Who is the Holy Spirit?' Stonecroft's Guide Book Lesson #2 in Swahili, the English version of Who is the Holy Spirit? is available online from Stonecroft's website.

This transforming study will reveal who Jesus is, what He does, and what life is like when He lives within you. Learn what the Holy Spirit does in the life of a Christian and how He can help you grow to be more like Christ. (6 lessons)

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #2 Swahili Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #2

Download Swahili Lesson #2 Student Study Book

 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us