Project Hope     home >> stonecroft>> je mungu yokoje? >> somo 1 >> somo 2
Je Mungu yokoje? - Somo #2
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club
Je Mungu yukoje?

Download Swahili Lesson #2 Student Study book page 1-2

Download Swahili Lesson #2 Student Study book page 3-4

Maombi

Mungu uishie milele, nakuabudu.nimejifunza kuwa haukuwa na mwanzo wa hautakuwa na mwisho, nasadiki kuwa wewe ni muumbaji wa kila kitu tukionacho. Naomba unisaidie kufikilia vizuri kuhusu wewe na neno lako,naomba katika jina la Yesu. Amen.

1. Kutumia maneno rahisi elezea unafukilia nini kuhusu Mungu, uwe mkweli na dhahili kuhusu jambo hili la kumhusu Mungu na jinsi unavyo mfikilia, katika mwisho wa masomo haya swari hili litaulizwa tena.
________________________________________________________________

Kujisomea Biblia kwa Juma

Kila siku katika juma hili jisomee neno la MUngu hili na elezea kila kipengele kinasema nini kumhusu Mungu.

1 Wakorintho 1:9
Je kifungu hiki kinasema nini kumhusu Mungu?
________________________________________________________________

Warumi 16:27
Neno hili linamuelezeaje MUngu?
________________________________________________________________

Luka 1:37
Neno hili linatuambia nini kuhusu Mungu?
________________________________________________________________

Yohana 3:16
Je neno hili linasema nini kumhusu Mungu.
_______________________________________________________________

Hesabu 23:19
Ni sifa zipi za Mungu zimetajwa?
_______________________________________________________________

Ufunuo 15:3-4
Je ni sifa zipi za Mungu zinatajwa hapa?
_______________________________________________________________

Ufunuo 1:8
Je hili nalo linasema nini kuhusu Mungu?
_______________________________________________________________

. Chagua kifungu ambacho kinaleta maana zaidi kwako katika vifungu vya kujisomea vya juma, tafakari ukweli huo unamaana gani katika maisha yako na utendee kazi.

Mungu hana mwili kama tulivyo sisi, tukifikilia hivyo tutakuwa tunafanya kosa kubwa sana maana tutafikilia kuwa Munguana mapungufu kama tulivyo sisi wanadamu.

Hatukujiumba wala hatukuumba hata upepo, chakula, au maji, ambavyo tunaviihitaji ili maisha yetu yasonge mbele. Lakini Mungu huishi kama yeye na haitaji msaada wowote ili maisha yake yapate kusomnga mbele

.Kila kitu tukionacho katika dunia kilifanywa au kuumbwa lakini yeye Mungu hakuumbwa, wala hakufanywa huyu Mungu ni tofauti kabisa na vitu tuvionavyo yeye NDIYE, yeye amekuwako na atakuwako yeye yupo milele na huishi milele.

Jambo jingine la kumtofautisha Mungu na sisi ni kwamba yeye ni Roho wakati sisi husihi katika mwili.

2. Je Yohana 4:24 inasema kumhusu Mungu?

(If you do not have a Bible, look up the verses in the Bible Verse Handbook)

Download Bible Verses Handbook

Mungu wetu hazuiliwi na kitu

Sulemani aliomba.

“Lakini Mungu je atakaa kweli kweli juu ya nchi? Mbingu hazikutoshi wala mbingu za mbingu sembuse hii nyumba niliyo ijenga!”
1 Wafalme 8:27

Je wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu?
Waweza kuufikilia upeo wa huyo mwenyezi?
Ni juuu mno kama mbingu waweza kufanya nini wewe?
Ni wenye kina kuliko kuzimu waweza kujuoa nini wewe?
cheo chake ni kirefu kuliko dunia
Ni kipana kuliko baharo
Ayubu 11:7-9

Nizaidi ya upeo wetu

Mungu huunguruma kwa kustaaajabisha kwa sauti yake;
Hufanya mambo makuu ambayo hatuwezi kuelewa.
Ayubu 37:5

“Maana mawazo yenu si mawazo yangu,
Wala njia zenu si njia zangu” asema BWANA.
“Maana kama mbingu zilivyo juusana kuliko nchi,
Kadharika nia zangu zi juusana kuliko niia zenu,
Na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.”
Isaya 55:8-9

3. Sifa za kiroho ndizo sifa za kweli zimhusuzo Mungu,kila kifungu utakachosoma hapa kina sifa

Ya Mungu soma na andika sifa hiyo mbele ya kifungu

a. 1 Yohana 4:8 ____________________________________________________________
b. 2 tesalonike 3:3 ____________________________________________________________
c. Yakobo 1:17 _____________________________________________________________
d. Marko 10:18 _____________________________________________________________
e. Waebrania 1:8 _____________________________________________________________
f. Luka 1:78 _____________________________________________________________
g. 1 Petro 1:15-16 _____________________________________________________________

Sifa za Mungu

Mungu ni Upendo
Upendo ni sifa ya Mungu lakini sio tafsiri ya Mungu, inaelezea MUngu jinsi alivyo kama sifa nyingine zinavyoelezea, uaminifu, uzuri, huruma, haki, utakatifu, zote hizi zinaeleza Mungu alivyo.

Yeye ni kila kitu kilichotajwa hapa chini na wakatai huo huo upendo wa Mungu mara zote ni mzuri na mtakatifu,wa uamini fu na wa haki.

Mungu ni mwaminifu
Tunaweza kumtegemea Mungu wetu maana ni mwaminifu na hutunza agano lake mara zote, tunaweza kuishi kwa matumaini ya hata kesho maana Mungu ni mwaminifu.

Mungu habadiriki
Moja ya sifa za Mungu ambazo bado hatujazisema ni kwamba Mungu habadiriki, tunjua kuwa Mungu wawezi kutokuwa mwaminifu maana hili litamfanya abadirike. Malki 3:6

Mungu ni mwema
Huu wema wa Mungu ni tofauti na wema wetu maana Mungu ni mwema katika kila jambo ambalo analifanya tofauti na wanadamu. Yesu alisema Mungu pekee ndiye aliye mwema. Zaburi 107:1

Mungu ni wa haki
Mungu atendapo haki hatendi haki kama kumtuliza au kumpongea mwanadamu kwa yale aliyotenda bali hutenda haki kama yeye jinsi alivyo, Mungu ni Mungu na ataendelea kuwa Mungu hawezi akawa kitu kingine zaidi ya kuwa Mungu Kumbukumbu la Torati 32:4

Mungu ni wa huruma
Huruma ni sifa mojawapo ya Mungu na mara zote huyu Mungu amejawa na huruma na pia pamoja na huruma na pia yeye ana haki, hata atendapo haki hua na huruma pia, huwa anaonyesha huruma isiyokuwa na kipimo mara zote anaposhughulika na mwanadamu, hii huruma sio ya kitambo tu bali ndivyo Mungu alivyo, Mungu alikuwa na huruma hata kabla nyakati za muda hazijaanza na ataendelea kuwa na huruma, soma 2 Wakorintho 1:3

Mungu ni mtakatifu
Huu utakatifu unajitegemea,ni wabila mawaa,ni wa tofauti na ni mkuu sana,utakatifu wa Mungu unapita hata fahamu zetu,utakatifu wa Mungu hupita fahamu zote na huu utakatifu anao yeye mwenyewe.

4. a Mungu anahitaji wakristo wafanye nini?
1 Petro 1:13-16
______________________________________________________________

b.Kutokana na msingi wa 1 Wakorintho 1:30 tunawezaje kuwa
kuwa watakatifu.
______________________________________________________________

BWANA asema hivi mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake, bali ajisifu kwa sababu hii kwamba ananifahamu mimi, na kunijua kuwa mimi ni BWANA nitendaye mema, na hukumu, na haki katika nchi, maana mimi napendezwa na mambo hayo asema BWANA.
Yeremia 9:23-24

Sifa taytu za tofauti

Mungu ana nguvu zote aliviumba vyite vitu vionekanavyo na visivyo onekana kwa kutamka tu neno lake, ana vitawala vyote na ana nguvu za kutendea miujiza na ndio maana tunasema Mungu ana nguvu zote - Ominipotent.

Mungu huyajua mambo yote, hakuna jambo asilo lijua hivyo nguvu za Mungu na ufahamu wake huwezi ukavitenga, tunaliita jambo hili Omniscient.

Mungu yupo popote katika muda mmoja, anapatikaka popote katika muda huo huo mmoja, tunasema yeye ni - Omni present.

5. Soma vifungu hivi vifuatavyo na andika katika vifungu hivyo ni sifa gani ya Mungu inazungumziwa hapo. Omnipotence,omnipresence,omniscience.

“……….na ntakuwa nanyi mpaka mwisho wa dahari.”
---------Mathayo 28:20


“……Mimi ni Mungu mkuu….Je kuna jambo gumu la kumshinda BWANA?”
---------Mwanzo 17:1.18:14


“Hakuna jambo ambalo linajificha mbele za Mungu, kila jambo katika viumbe vyake vi wazi kabisa mbele zake,na kwake tu ndiko tutakako toa hesabu ya matendo yetu.”
---------Waebrania 4:13

MAOMBI
Mungu mwenye nguvu nashukuru yote niliyo jifunza ya kukuhusu.nashukuru kuwa unapatikana mahali popote, na pia una nguvu zote, na unatambua mambo yote.
Wewe ni Mungu wa ajabu. Nashukuru kuwa unawapenda na kuwaelewa watu ulio waumba.
Nakushukuru kwa sababu ya Baraka zetu zote, katika jina la Yesu. Amen.

This is a translation of Lesson #2 Students Study Book, the English version of - What is God like is available online from their website.

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

View Guidebook online

Download Swahili Lesson #2 Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #2

 

 
 

JE MUNGU YUKOJE?

 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us